Latest Updates

Mcheza mieleka wa zamani bingwa wa WWE ajiua kwa kujinyonga


Mcheza mieleka wa zamani wa WCW na WWE, Sean O’Haire amekutwa akiwa amefariki kwa baada ya kujinyonga, Jumanne wiki hii.
Kwa mujibu wa TMZ, polisi wameeleza kuwa walimkuta O’Haire akiwa chumbani kwake South Carolinaakiwa amejifunga kamba shingoni na tayari ameshakufa. Mwili wake ulitambuliwa kwa mara ya kwanza na baba yake ambaye aliwapiga simu polisi.
O’Haire ambaye jina lake halisi na Sean Hair aliingia katika ulimwengu wa mieleka kwenye WCW (World Championship Wrestling) mwaka 2000 na mwaka huo alipewa ubingwa wa ‘Rookie of the Year’.
Yeye na partner wake Chuck Palumbo waliwahi kuwa mabingwa wa WCW kabla ya kampuni hiyo kununuliwa na WWE.
Mwanamieleka huyo alifahamika zaidi kwa utambulisho wa sentensi yake mara kwa mara “I’m not telling you anything you don’t already know.”

0 Response to "Mcheza mieleka wa zamani bingwa wa WWE ajiua kwa kujinyonga"

Post a Comment