Latest Updates

WAGOSI WA KAYA KUSHIRIKIANA NA JUMA NATURE, ROMA



KUNDI la Wagosi wa Kaya ambalo lilikaa kimya kwa muda wa miaka 8 hivi sasa lipo katika mikakati ya mwisho ya kuandaa albamu yao huku wakiwa karibu na mashabiki yao ikiwa ni njia moja wapo ya kutumia mitandano ya kijamii ili kuweza kuliteka soko la burudani.
Katika kutumia njia ya mitandao ya kijamii kama moja wapo ya kuwa karibu na mashabiki wao kundi hili kupitia ukurasa wao wa Facebook ili wapendekeza majina ya wasanii ambao mashabiki wao wangependa kufanya nao kazi.
Baada ya kuomba mashabiki wawapendekeze ni wasanii gani ambao wangependa wafanye nao kazi ya muziki ikiwa ni nimbo moja ya kushirikiana.
Baada ya kupendekeza juzi, kundi hilo lilitoa matokeo kwa mashabiki wao huku ikionesha kuwa Juma Nature, pamoja na Roma ndio wasanii waliopendekezwa kwa wingi na baadhi ya mashabiki wao kufanya nao kazi ya muziki.
Kupitia ukurasa wao wa Facebook kundi hilo liliandika kuwa "wasanii ambao wamependekezwa sana ili tufanye nao kazi katika nyimbo ni pamoja na Juma Nature, Roma na wengineo wengi tu, naamini hatujawahi kufanya kazi na wasanii wengi ila kwa heshima yenu mashabiki tutashirikiana na hao mliowachagua na wengineo tutashirikiana nao na mtawasikia kwenye alamu yetu ya uamsho hatutawaangusha kamwe".

0 Response to "WAGOSI WA KAYA KUSHIRIKIANA NA JUMA NATURE, ROMA"

Post a Comment