Latest Updates

JAY Z KAWAANDALIA ZAWADI NONO KANYE WEST NA KIM


MWANAMUZIKI nyota wa miondoko ya Hip Hop Jay Z ambaye pia ni rafiki wa karibu na bwana harusi mtarajiwa Kanye West, imedaiwa kuwa hatohudhuria katika ndoa ya rafiki yake huyo ambayo inatarajiwa kufungwa hivi karibuni.
Sababu zinazopelekea Jay Z pamoja na mke wake kutohudhuria ndoa hiyo ni kutokana kwa sherehe hiyo kuoneshwa kwenye kipindi cha reality show ya Kim Kardashians ambaye ndiye mwanamke anayetarajia kufunga ndoa na Kanye.
Ndoa hiyo inatarajiwa kufungwa mwezi ujao jijini Paris Ufaransa chanzo kimoja kimedai kuwa Jay Z tayari ameshampa taarifa rafiki yake huyo kuwa yeye pamoja na familia yake hawataudhuria sherehe hiyo kutokana na sababu hizo.
Kwa mujibu wa gazeti la The Sun limedai kuwa Jay Z amepanga kuwafanya sherehe kubwa mara baada ya tukio hilo kumalizika ambapo sherehe hiyo ameipanga kuifanya New York ndani ya ukumbi wa 'Club 40/40.
Ambapo katika sherehe hiyo ya rafiki yake kipenzi amepanga kutumia  kiasi cha £100,000 katika honeymoon yao kama zawadi yake.

0 Response to "JAY Z KAWAANDALIA ZAWADI NONO KANYE WEST NA KIM"

Post a Comment