Latest Updates



HATIMAYE kifungu cha 57 fasihi ndogo ya 3 inayozungumzia nafasi ya waandishi wa habari kuruhusiwa kuingia katika vikao vya kamati ya Bunge Maalum la Katiba
imepitishwa na wabunge wa CCM huku wabunge wa Chadema akiachwa pasipo kujua cha kufanya.Hatua hiyo ni sawa na waandishi wa habari kuchinjiwa
Habarini huku wananchi wakinyimwa uhuru wa kupata habari kuhusu mambo yatakavyo endelea ndani ya vikao vya Bunge hilo.
Katika kile kinacho onekana kwamba ni njama za kuweka mambo katika hali ya usiri zaidi, katika mkutano wa Bunge Maalum la Katiba Mpya inayoendeloe mjini Dodoma
inaonyesha ni jinsi gani wabunge wa CCM walijipanga kufanya mambo kwa usiri na kuwanyima wananchi fulsa ya kujua mambo yanavyo endelea ndani ya vikao vyao
Akizungumzia suala hili Mjumbe wa kamati ya maandalizi ya rasimu za kanuni za bunge hilo George Simbachawene alipinga suala hilo kwa nguvu zote huku pia
akipingana hata na maamuzi yaliyotolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Professa Costerick Mahalu ambaye alitaka suala hilo liachwe wanza ili kamati yake ikaangalie namna nzuri ya kuwaruhusu wanahabari kuingia katika vikao hivyo.
Kitendo cha Simbachawene kushikilia msimamo huo inaleta tafisiri kwamba huo ndiyo mpango wa Chama Cha Mapinduzi uliokuwepo tagu mwanzo ya kuwataka wabunge wake
walijipange kufanya mambo yanayopaswa kuwa siri yafanyike kwa uwazi na yake yaliyopangwa kufanyika kwa uwazi yafanyike kwa usiri bila kujali kwamba wanavunja Katiba mama ambayo bado inatumika mpaka hivi sasa
Hoja za kuitaka bunge hilo kufuta mapendekezo ya kanuni katika kifungu cha 51 na 57 fasiri ndogo ya 3 inayompa mwenyekiti wa kamati haki ya kutoa ufafanuzi kwa
waandishi wa habari juu kilichozungumzwa na kamati, badala ya kuruhusu waandishi waingie na kusikiliza kinachojadiliwa wenyewe na kuwaeleza
wananchi wengine ilipigwa na Wabunge Halima Mdee Chadema ,Amos Machari NCCR-Mageuzi,Ester Bulaya CCM,Maria Sarungu na Ezekiel Oluoch wote wateule wa Rais Kikwete.

0 Response to " "

Post a Comment