Latest Updates

KATIKA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI WATANZANIA WAONGOZA KUSHEREHEKEA SIKU YA WAPENDANAO,



IKIWA kila ifikapo Februari 14 ni siku ya wapendanao duniani, utafiti uliofanywa na shirika la Ipsos, lenye lengo la kujua ni nchi gani ya Afrika Mashariki inayoongoza kwa kuilewa siku hiyo ya wapendanao.
Utafiti huo ulilenga watu wenye umri wa zaidi ya miaka 18 katika miji mikubwa ya nchi tatu Kenya, Uganda pamoja na Tanzania ili kujua uelewa kuhusu suala zima la siku ya Mtakatifu Valentine.
Waliohojiwa ni jumla ya watu 528 kutoka Tanzania, 1050 Kenya na Wangana 1006, ambapo utafiti huo ulizingatia jinsia, wanawake na wanaume, mahojiano hayo yalifanywa kwa kutumia msaada wa computer na simu.
Katika nchi hizo tatu utafiti ulifanywa tarehe 7 hadi 10 mwezi februari 2014
Katika utafiti huo umebaini kuwa Tanzania kwa ujumla wake na nia ya siku hiyo wanaume ndio wanania ya kusherehekea zaidi siku hiyo kuliko wanawake 
Kwa mujibu wa tafiti hizo kwa nchi hizo tatu tanzania imepata asilimia 72 inayoamini kuwa siku hii itakuwa ya mashamsham ya mapenzi zaidi kuliko nchi nyingine ambapo Uganda imepata asilimia 56, kenya inaasilimia 52.
Inadaiwa pia siku hii ya wapendanao, matumizi yanabadilika ambapo wataznania wamepata asilimia 42, kutegemea  kununua nguo kuliko vitu vingine  wakati Uganda  inaasilimia 37, pamoja na Kenya asilimia 36 kununua maua zaidi.

0 Response to "KATIKA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI WATANZANIA WAONGOZA KUSHEREHEKEA SIKU YA WAPENDANAO,"

Post a Comment