Latest Updates

WAKAZI KUWASUPRIES MASHABIKI WAKE LEO USIKU



Baada ya kuachia Mixtape yake aliyopa jina la 'Utatu Mtakatifu' msanii wa muziki wa kizazi kipya miondoko ya Hip Hop nchini, Webiro Wassira 'Wakazi' leo usiku anatarajia kuwasupries mashabiki wake kwa kuachia nyimbo yake mpya ambayo haijajulikana ni wimbo gani.

Akizungumza na Pro-24 kwa njia ya simu Wakazi alieleza kuwa anatarajia kuachia nyimbo hiyo kama supries kwa mashabiki wake huku akikataa kueleza jina la wimbo huo na sababu za kufanya hivyo.

Pamoja na hayo msanii huyo anatarajia kusafiri kwenda nchi ya mbali kwa ajili ya kukamilisha mipango yake ya kuendeleza muziki wake kuweza kuvuka mipaka ya nje ya Tanzania.

0 Response to "WAKAZI KUWASUPRIES MASHABIKI WAKE LEO USIKU"

Post a Comment