Wasanii wa muziki wa bongo fleva wanaounda kundi la Makomando Fred
Felix 'Fred Wayne', pamoja na Said Christopher 'Mucky' wamedai kuwa nyimbo yao
mpya inayokwenda kwa mtindo wa 'kibabababa' imebadilisha mfumo wa maisha yao
pamoja na kuwaongezea mashabiki lukuki.
Akizungumza na jarida hili Fred Wayne amedai kuwa nyimbo hiyo
imepokelewa vyema na mashabiki hali iliyopelekea kupata shoo nyingi kwa kipindi
hiki cha mwezi huu wa kwanza ingawa ni mwezi mgumu kufanya shoo.
Kutokana na hilo amesema kuwa kundi hilo limezidi kung'aa kwa
kufanya shoo nyingi kwa mwezi huu, huku wakiendelea kupokea mialiko ya kufanya
shoo mbalimbali kwa kipindi cha miezi 5 mfululizo.
Ameeleza kuwa kuendelea kupata shoo nyingi hizo ni kutokana na
nyimbo yao hiyo kuendelea kufanya vizuri ambapo nyimbo hiyo sasa inamwezi tangu
imeachiwa lakini imeonekana kufanya vizuri.
"Hii nyimbo ya mtindo wa kibababa imetubadilisha vitu vingi kwenye
soko la muziki sasa nyimbo yetu inatuuza kwa kipindi hiki tumeona mabadiliko
mwengi na bado inaendelea kiufanya vizuri" alisema Fred.
Alieleza kuwa siri ya kufanikiwa kwenye muziki ni kuwa mbunifu
hususani katika kutunga mashairi na kutengeneza video yenye ubora huku
mtayarishaji wa muziki kuendelea kuwa mbunifu katika kuchanganya vyombo.
0 Response to "'KIBABABABA' YABADILISHA MTINDO WA KUNDI LA MAKAMANDO "
Post a Comment