Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Kilimanjaro, Michael
Mwita (Kushoto)
akiteta jambo na Mgombea wa kiti cha Udiwani
kata ya Kibor0loni kwa
tiketi ya chama cha Mapinduzi, Willy
Adriano, wakati wa Uzinduzi wa
Kampeni kuelekea uchaguzi
mdogo kuziba pengo lililoachwa wazi na
aliyekuwa Naibu Meya
na Diwani wa Kata hiyo,, Marehemu Vincent Rimoy
aliyefariki
dunia Novemba 6, mwaka jana.

(aliyeshika kipaza sauti), akimnadi mgombea wa CCm katika Uchaguzi
mdogo wa Udiwani, Wlly Adriano katika uchaguzi uzinduzi wa kampeni za
uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Februari 9 mwaka huu kuziba pengo
lililoachwa wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa Diwanbi wa Kata ya
Kiborloni, Vincent Rimoy, alyefariki dunia ghafla Novemba 6 mwaka
jana.

…………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu,
Moshi
CHAMA cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mwishoni mwa wiki walifanya uzinduzi
wa Kampeni za uchaguzi
mdogo wa udiwani katika kata ya Kiboriloni liliachwa wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo, Vincent Rimoy (CHADEMA), aliyefariki ghafla Novemba 6 mwaka jana.
mdogo wa udiwani katika kata ya Kiboriloni liliachwa wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa diwani wa kata hiyo, Vincent Rimoy (CHADEMA), aliyefariki ghafla Novemba 6 mwaka jana.
Wa kwanza kufanya uzinduzi ni Chadema,
waliozindua kampeni yao kwa mbwembwe wakimtambulisha mgombea wao, Frank
Kagoma ambaye ni mwenyekiti wa mtaa wa Mnazi, uzinduzi
ulioongozwa na viongozi mbalimbali wa ngazi za juu wa chama hicho
mkoani hapa akiwemo mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Kilimanjaro na
Mbunge wa Jimbo la Moshi mjini, Filemon
Ndesamburo.
Wakizungumza katika Nyakati tofauti katika
uzinduzi huo uliofanyika, Jumamosi ya Januari 18, mwaka huu, katika
stendi ya kidia, viongozi wa Chadema walianza kumnadi mgombea wao ambap[o
walimtaja kama mtu sahihi ambaye anaweza kuendeleza mapambano ya chama
hicho ndani ya baraza la madiwani kupinga ufisadi na uonevu katika
manispaa ya Moshi.
Meya wa Manispaa ya Moshi, Jafari Michael,
aliwataka wananchi wa kata hiyo kumchagua mgombea wa Chadema kwani ndiye
mwenye uwezo wa kutekeleza yale yote aliyoyaanzisha Marehemu
Rimoy ndani ya kata hiyo na baraza la
madiwani.
“Wananchi wa kiboriloni msidanganyike, chaguo
la kweli katika maendeleo ya kata hii ni Kagoma, katika kipindi
chake kama mwenyekiti Kagoma alifanikiwa kuvunja magenge yote ya
ujambazi na sasa mnatembea
vifua mbele bia wasiwasi, tupeni kagoma
tuendeleze moto wa Chadema ndani ya Baraza la Madiwani, tupeni kagoma
tukamalizie kazi aliyoianzisha Rimoy,” alisema
Rimoy.
Naye Mbunge wa Jimbo la Moshi mjini, Filemona
Ndesamburo alisema kazi ya kuleta maendeleo katika kata hiyo na mkoa
kwa ujumla unaweza kufanywa na watu makini wenye uthubutu kama
alivyo na uthubutu Mgombe wa kiti hicho, Frank
Kagoma.
Kwa upande wao, Chama cha Mapinduzi CCM,
waliofanya uzinduzi wao juzi, kwa kumtambulisha mgombea wa kiti hicho kwa
tiketi ya CCM, Wlly Adriano walisema Maendeleo ya kata ya Kiborloni
ni zaidi ya itikadi za siasa na kuwataka wananchi wa kata hiyo kufanya
uamuzi sahihi.
Akizungumza na maelefu ya wananchi
waliojitokeza katika viwanja vya stendi ya Kidia, Katibu wa CCM mkoa wa
Kilimanjaro, Steven Kazidi alisema wapo baadhi ya wanasiasa ambao wamekuwa
wakitafuta madaraka kwa njia mbalimbali, ikiwemo kufanya vurugu na
maandamano.
“Unajua ukisikia nchi fulani ina maendeleo
kiuchumi, kisiasa na mambo mengine ni kwa sababu kuna amani, kwa hiyo hili
jambo ndugu zangu ni muhimu sana kulizingatia ili kutuwezesha
kuendelea na kazi zetu za kijamii vizuri” alisema
Kazidi.
Kwa upande wake Mchumi wa CCM mkoa wa
Kilimanjaro, Paul Matemu, aliwataka vijana kutokuuza shada zao za
kupigia kura kwani kufanya hivyo ni kuuuza maendeleo
yake.
Aidha Matemu aliongeza kwa kusema kuwa siasa
bila maendeleo hakuna kujenga msingi wa kuleta maendeleo, na kuwataka
wananchi wa kata ya kiboriloni kuchagua Willy Adriano ili aweze
kuwawakilisha katika baraza la madiwa la Manispaa ya
Moshi.
Naye Mgombea udiwani kwa tiketi ya chama hicho,
Willy Adriano, alisema Siasa za Tanzania haziwezi kupiga hatua endapo
wananchi hawatabadilika na kuacha tabia ya kuchaguana kwa kuangalia
kigezo cha itikadi za kisiasa.
Uchaguzi mdogo wa udiiwani katika kata ya
Kiboriloni uunarajiwa kufanyika Februari 9 mwaka huu kuziba pengo
lililoachwa wazi
0 Response to "CCM NA CHADEMA WAZINDUA KAMPENI YA UCHAGUZI MDOGO WA UDIWANI KIBORILONI "
Post a Comment