Latest Updates

WAKAZI KUZINDUA 'TOUCH'


Msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini anayeimba miondoko ya Hip Hop Wakazi kesho anatarajia kuzindua video wa wimbo wake unaojulikana kwa jina la 'Touch' ambayo aliitumbuiza kwa mara ya kwanza nchini Afrika Kusini katika Big Brother The Chase.
Msanii huyo katika uboreshaji wa kazi yake hiyo ameamua kuvujisha wimbo ambao hakuwa rasmi alioupa jina linalojulikana 'Wanawake wa Dar'.
Nyimbo hiyo ambayo inapatikana katika mixtape yake inayojulikana kwa jina la 'I am Afrika Mixtape' inatarajia kutoka hivi karibuni.
Akielezea sababu za kuivujisha nyimbo hiyo ya wanawake wa Dar alieleza kuwa anaamini kuwa itafanya vizuri huku nyimbo yake ya 'Touch' kuendelea kufanya vizuri zaidi katika vituo vya radio kwa sasa.

0 Response to "WAKAZI KUZINDUA 'TOUCH' "

Post a Comment