MSANII wa filamu na muimbaji wa bongo fleva nchini Baby Joseph 'Beiby
Madaha' amepata 'shavu' la kufanya show nchini Uingereza mwishoni mwa
mwezi huu, huku akiendelea kuitangaza bidhaa yake ya manukato
yanayozalishwa na kampuni ya muziki ya Candy & Candy iliyopo nchini
Kenya.
Ndani ya show hiyo ambayo inatarajia kufanyika Novemba 30, msanii huyo
pia atapata nafasi ya kuendelea kuitangaza bidhaa zake ikiwemo manukato
pamoja na mifuko ya kubebea vitu mbalimbali ikiwemo CD.
Mwanadada huyo amebainisha kuwa tangu aingia mkataba na kampuni hiyo ya
nchini Kenya ameweza kupiga hatua kwenye kazi yake ya muziki hali
ambayo kwake anaona ni njia nzuri ya kufikia maendeleo.
Madaha amedai kuwa ndani ya show hiyo mashabiki wake watapata nafasi ya
kupata zawadi ya bidhaa hizo ambapo zitazinduliwa tena nchini humo kabla
ya kumaliza show hiyo.
Alieleza kuwa bidhaa hizo ni moja ya kazi zake ambapo bado anajipanga
kuendelea kufanya vitu vikubwa zaidi katika biashara na kazi zake za
muziki.
Mbali na kuzindua bidhaa hizo hivi karibuni msanii huyo alitoa zawadi za
bidhaa hizo kwa baadhi ya mashabiki wake mitaanii ambapo alitoa kwa
wanawake na watoto ili kuonesha upendo kwa mashabiki .
0 Response to "BEIBY MADAHA APATA SHAVU UINGEREZA "
Post a Comment