Home » Uncategories » Batuli "awa-diss" waigizaji na mashabiki wanaoandika matusi kwenye mitandao ya kijamii
Batuli "awa-diss" waigizaji na mashabiki wanaoandika matusi kwenye mitandao ya kijamii
Mwigizaji Yobnesh Yussuph maarufu kama batuli
ameamua kuwatolea uvivu waigizaji wanaoandika matusi kwenye mitandao na
kuwaambia kuwa badala ya wao kupoteza muda huo kutukana matusi makali
kwenye mtandao wangetumia muda huo kufanya Ibada ili wakifa waende
peponi kwa Amani ambako wangeweza kupajaza mpaka wengine wakose viti. “…Ule muda watu wanaoutumia kuandika naneno makali (MATUSI)
kwenye instagram (Mtandao wa kijamii) wangekuwa wanautumia kwa ibada
peponi kungejaa..” Alisema batuli.
Huku ikiwa bado haijajulikana anamlenga nani moja kwa moja na
ujumbe huo baadhi ya wachunguzi wa mambo wamehusisha kauli hiyo na
kitendo kilichotokea juzi cha mwanadada wa bongomovies kuporomosha matusi makali sana kwenye mtandao huo maarufu wa kijamii nchini.
0 Response to "Batuli "awa-diss" waigizaji na mashabiki wanaoandika matusi kwenye mitandao ya kijamii"
Post a Comment