Latest Updates

Picha 11 za jinsi huyu anaetuhumiwa kuwa tapeli anaetumia jina la Jokate Mwegelo alivyokamatwa

Aliefanikisha huyu jamaa kukamatwa ni mrembo mmoja model Blessing ambae alishiriki Miss Morogoro 2013 ambapo namkariri akisema “wiki mbili zilizopita nilipata msg kwamba Kidoti hair na Mzinga Planet wanahitaji mamodo kwa ajili ya kutengeneza matangazo kwa ajili ya nywele za kidoti, tulikua Morogoro kwa ajili ya Miss Morogoro tukaja Dar mpaka Mzalendo Pub msg ilipotuelekeza lakini nilivyoingia sikuona mtu ambae anahusiana na Jokate, niliona watu ambao nawajua lakini sio kuhusu nywele’ ‘Nikampigia kaka mmoja anaitwa Johnson kwa sababu najua anafahamiana na Jokate, nikampigia kumfokea kumwambia nyinyi vipi mbona mmetangaza audition alafu sioni hata mtu mmoja ambae anahusika? naona watu ambao kampuni zao zipo majumbani kwao? baada ya dakika zaidi ya 10 kina Jokate wakawa wameshafika japo baadhi ya mamodo wengine walikua wameshaondoka lakini baadhi ya viongozi kama Majaji wa kike walikuepo na walipoulizwa wakasema tumsubiri Mpeka ambae ndio muhusika na pia Mkurugenzi wa Mzinga Planet” – Blessing Baada ya kina Jokate kufika Mpeka alipigiwa simu ili arudi Mzalendo Pub, japo alisita sana mtuhumiwa huyu alikuja kwenye eneo la tukio na kukutana uso kwa uso na Jokate na timu yake, baada ya hapo akaanza kusingizia kwamba yeye hausiki ila kuna watu wengine ndio wanahusika ila alipotoa namba zao wakapigiwa simu, kila mmoja alionekana kutaharuki kwa sababu hawajui chochote kuhusu hiyo Mzinga Planet. Baada ya Jokate na timu yake kukaa na Mpeka na kumuuliza kistaarabu bila kutoa ushirikiano wa kutosha, uamuzi ulitoka kwamba apelekwe Polisi Osterbay ili kuendelea na taratibu nyingine za kisheria. Mpeka alikua anaonekana analia wakati mwingie na hiyo ilikua ni baada ya kumpiga huyu msichana shuhuda aitwae Blessing kwa sababu alimchomea mpaka akakamtwa.
Jokate amesema “miongoni mwa mabinti waliowahi kutapeliwa na matapeli wanaotumia jina la Jokate Mwegelo au Kidoti ni pamoja na mrembo mmoja alipelekwa kwenye hoteli Arusha ambapo mwanaume alimwambia kama atalala nae hotelini atapata fursa ya kuwa model wa Kidoti, alilala nae siku tatu hotelini alafu baadae mwanaume akaondoka ghafla na kuiba simu za huyu mrembo na laptop na hata bili akamwachia yule msichana ndio alipe” Hii audition aliyoifanya Mpeka, usaili mdogo ambao ni Wasichana takribani arobaini walijitokeza, ‘mtu akisikia tangazo kama hili au kama nikiwa na kitu ofcourse watu watakisikia kwenye Amplifaya au millardayo.com na pia niko twitter @JokateM kwa hiyo itakua ni rahisi kutambua kweli kama hiki kitu kimetoka kwa Jokate’
by millardayo.com

0 Response to "Picha 11 za jinsi huyu anaetuhumiwa kuwa tapeli anaetumia jina la Jokate Mwegelo alivyokamatwa"

Post a Comment