Melissa ambaye ni mtoto wa muigizaji na mkosoaji maarufu wa mavazi
kupitia vipindi vya runinga, Joan Rivers amepanga kumfungulia mashitaka
daktari aliyemtibu mama yake kabla hajapatwa na umauti.
Melissa
mwenye umri wa miaka 46 amepanga kumshitaki Dr Gwen Korovin ambaye
alidaiwa kutokuwa na kibali cha kufanya kazi za utabibu katika Yorkville
Endoscopy Clinic huko Manhattan ambapo Joan Rivers alifariki akiwa na
umri wa miaka 88.
Rafiki wa karibu wa Melissa ameiambia MailOnline kuwa Melissa yuko serious na mpango huo.
Amesema ingawa ni vigumu sana kujadili nae kitu kinachomuudhi wakati huu, lakini ataanzisha mashtaka hivi karibuni.
Taarifa
zimeeleza kuwa daktari huyo licha ya kutokuwa na kibali bado anaendelea
kutoa matibabu katika hospitali hiyo wakati ambapo bado anachunguzwa na
vitengo vya usalama vya Marekani.
DAKTARI ASHTAKIWA KWA KUSABABISHA KIFO CHA MUIGIZAJI MAARUFU
Posted by Unknown
on Tuesday, October 7, 2014,
Add Comment
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Response to " DAKTARI ASHTAKIWA KWA KUSABABISHA KIFO CHA MUIGIZAJI MAARUFU"
Post a Comment