Latest Updates

LIL WAYNE KUSIMAMA KUFANYA MUZIKI?


MWANAMUZIKI kutoka Marekani Lil Wayne ameweka wazi msimamo wake wa kuacha kurekodi tena albamu, huku akieleza kuwa albamu yake ya mwisho itakuwa 'The Carter V'.
Alisistiza kuwa hiyo huenda ndio ikawa ni albamu yake kubwa ya mwisho kama msanii, ingawa haikuwekwa wazi sababu za msanii huyo kueleza kusimama kurekodi tena albamu.
Katika mahojiano na MTV, Lil Wayne alieleza kuwa hiyo ndio itakuwa albamu ya mwisho kurekodi ingawa alidai kuwa atakaa muda mrefu bila ya kufanya kazi ya kurekodi albamu nyingine.
Huku akiweka wazi kuwa endapo atatakiwa kurekodi albamu nyingine tena atafanya hivyo lakini kwa kiasi cha dola 25,35 ikiwa ni moja ya makubaliano yake na hao watakaotaka kufanya naye hiyo kazi.
Kauli hiyo si ya mara ya kwanza kusikia akisema kuacha kufanya kazi ya muziki, ikumbukwe kuwa Wayne alishawahi kujitangaza kuacha kufanya kazi hiyo June 2013.

0 Response to " LIL WAYNE KUSIMAMA KUFANYA MUZIKI?"

Post a Comment