
Chege Chigunda ni moja kati ya wasanii walikaa kwa mrefu
kwenye game la bongo fleva na kuwa juu kila anapotoa ngoma ama
anaposhiriki kwenye miradi ya muziki ya kundi lake au anapofanya mradi
wake mwenyewe.
Akiongea katika kipindi cha The Playlist cha 100.5 Times Fm na Omary
Tambwe, Chege ameyaelezea mafanikio aliyoyapata kwenye muziki kuwa ni
mafanikio makubwa kwake zaidi hata ya kununua meli.“Mafanikio yapo kwa sababu kwanza namshukuru Mungu mimi naishi kutokana na muziki peke yake sifanyi kitu kingine chochote. Naiendesha familia yangu, namtumza mama yangu mzazi, kwa hiyo ni mafanikio makubwa sana kuliko ningenunua meli sio..”
Katika hatua nyingine, Chege alieleza kuwa ataachia wimbo wake mpya hivi karibuni ataachia wimbo mpya alioupa jina la ‘Waue’
MSIKILIZE HAPA
Audio
.http://www.hulkshare.com/y2zaytskgem8
0 Response to "Chege ayaelezea mafanikio aliyopata kwenye Muziki ni zaidi ya kununua meli "
Post a Comment