Latest Updates

BAADA YA KUGUNDUA UZITO WAKE UMEONGEZEKA, RICK ROSS ABADILI MFUMO WA MAISHA


MSANII wa miondoko ya Hip Hop kutoka nchini Marekani Rick Ross ameamua kubadilisha mfumo wake wa maisha ili kuzuia matatizo mbalimbali yakiwemo kuugua, pamoja na kuboresha afya yake.
Rapper huyo amebadilisha mfumo wake wa kula na jinsi anavyoishi ili kuupa mwili wake afya njema na kujizuia na magonjwa yakiwemo ugonjwa wa moyo.
Miaka miwili iyopita ilishawahi kuripotiwa kuwa rapper huyo alishawahi kupoteza fahamu akiwa kwenye ndege akielekea Florida hali iliyopelekea kusabababisha ndege hiyo kutua ili apatiwe huduma.
Alifanyiwa uchunguzi na kubainika kuwa uzito wa mwili wake na kukosa usingizi wa kutosha ndio ulisababisha hali hiyo.
Baada ya hali hiyo ameamua kubadili mfumo mzima wa maisha yake ambapo anafanya mazoezi mara mbili kwa siku, huku akila chakula kwa ajili ya afya na kupata muda wa kupumzika.
Pamoja na hayo alifanya maojiano na kutangaza ujio wake wa albamu yake mpya .

0 Response to "BAADA YA KUGUNDUA UZITO WAKE UMEONGEZEKA, RICK ROSS ABADILI MFUMO WA MAISHA "

Post a Comment