Latest Updates

COCA COLA WAANDAA TAMASHA LA BURE



KAMPUNI ya kutengeneza vinywaji baridi Tanzania Coca Cola, yazindua kampeni ya 'Good Time ya Ukweli na Coca Cola' yenye lengo la kuwapa fursa vijana kupata burudani ya muziki pamoja na michezo mbalimbali itakayotoa fursa ya kushinda zawadi mbalimbali.
Kampeni hiyo itaambatana na kutoa burudani ya muziki kwa vijana katika mikoa mbalimbali ikiwemo Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Arusha pamoja na mjini Moshi kwa kuwatumia wanamuziki nyota wa hapa nchini.
Ambapo baadhi ya wanamuziki watakaotoa burudani hiyo kwa vijana ni pamoja na Diamond Platanum, John Makini, Madee pamoja na Vanesa Mdee.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Saalam, Meneja wa kinywaji hicho cha Coca Cola Tanzania, Maurice Njowoka alisema kuwa, burudani hizo zitafunguliwa rasmi Februali 16 mwaka hii katika ufukwe wa Coco Dar es Saalam ambapo msanii Diamond , Vanessa Mdee, Madee pamoja na Joe Makini watafanya shoo.
"Lengo la burudani hizo ni kutoa fursa kwa vijana kufurahi pamoja na marafiki huku wakiburudika na Coca Cola, ambapo burudani hiyo inatolewa bure kwenye mikoa yote " alisema Njowoka.
Alieleza kuwa burudani hizo zitafanyika sehemu mbalimbali huku wakazi wa Mwanza watafanya katika viwanja vya Furahisha, ambapo mkoani hapo wanaume TMK, pamoja , Diamond pamoja na Madee watatumbuiza tamasha hilo mkoani huko, 
Ambapo alidai kuwa mfululizo wa burudani hiyo utazunguka katika miko hiyo huku baaadhi ya wasanii hao wakiendelea kutoa burudani ya bure kwa mashabiki wao

0 Response to "COCA COLA WAANDAA TAMASHA LA BURE"

Post a Comment