Yuster
Nyakachara ukilisikia jina hili kwa sasa unaweza ukajiuliza mara tatu
tatu,Huyu ni Nani?na anatokea wapi?Basi Yuster Nyakaracha ni dada wa
kitanzania mwenye malengo na anataka kuifikisha mbali sanaa yetu ya
filamu za kitanzani.Kwa miaka takribani 10(kumi)mwanadada huyu amekuwa
akizunguka dunia kwa ajili ya maonyesho mbalimbali ya sanaaa hasa ngoma
za asili ya kitanzania.Kupitia sanaa hiii ya ngoma za asili kumemfanya
kutembelea nchi zote za ukanda wa scandinavia ambazo ni
sweden,finland,denmark,norway na zingine zote.Kutokana na safari hiyo
ndefu ya takribani nchi kumi duniani ameweza kujifunza mambo mengi sana
kuhusu sanaaa na ngoma na uigizaji,iliyompelekea kupata uzoefu wa
kutosha katika sanaa ya filamu.
Kwa
sasa mwanadada Yuster nyakachara amerudi nchini Tanzania na kuamua
kufungua kampuni yake ya kutengeneza filamu aliyoipa jla la "EAGLE ENTERTAINMENT"kupitia
kampuni hii mwanadada Yuster ni miongoni mwa watakaofanya vizuri sana
kwenye sanaa ya soko la filamu za kitanzania.Hivyo basi mwanadada Yuster
amewaomba wadau wote wa sanaa nchini Tanzania kushirikiana naye ili
kuifikisha sanaa yetu mbali na hatimaye kufanikiwa kufahamika kimataifa
kama wenzetu Ghana,Nigeri na zambia.Mtandao wetu ulipofanya mahojiano
naye na kumuuliza je amejiandaaa vipi kukabiliana na soko la movie la
Tanzania kwa kuwa kuna kampuni nyingi za kutengeneza movie?Yuster
alijibu kwa umakini sana najua kuna makpuni mengi sana ya kutengeneza
movie Tanzania lakini akasema yeye ameamua kuanzisha kampuni hii ya
EAGLE ili kuleta ushindani katika utengenezaji wa filamu na hivyo
kupelekea makapuni kutokulala kwa kujiamini wanaweza,Akaendelea kusema
kuwa anajiamini kwa uzoefu wa takribani miaka 10 atafanya vizuri na
kuweza kufanya mapinduzi katika sanaa ya Filamu za kitanzania,Hivyo basi
tumpe sapoti mwanadada huyu ili aweze kuinua sanaa yetu.
DUHHHH WEKA SOURCE BASIII ULIPOTOA HABARI
ReplyDelete