>>MSHINDI
WA TATU: KILI STARS v ZAMBIA!!
>>ZOTE
NYAYO STADIUM, NAIROBI, DESEMBA 12!
FAINALI ya CHALENJI CUP itakuwa kati ya Wenyeji
Kenya na Sudan baada ya leo kuzibwaga Kilimanjaro Stars na Zambia kwenye Nusu
Fainali.
Kenya waliifunga Kilimanjaro Stars Bao 1-0 katika
Mechi iliyohamishwa toka Machakos na kupelekwa Nyayo Stadium, Nairobi baada ya
Uwanja kufurika maji.
Hata kuko Nyayo Stadium, Mechi hiyo ilichezwa
kwenye mvua na Kenya kufunga Bao lao la ushindi katika Dakika ya 4 kwa Bao la
Clifton Miheso.
Katika Nusu Fainali nyingine, Zambia na Sudan
zilitoka 0-0 katika Dakika 90 na Mechi kuongezwa Dakika 30 ambapo Sudan
walishinda 2-1.
Zambia walitangulia kufunga katika Dakika ya 110,
Mfungaji akiwa Ronald Kampamba na Sudan kusawazisha Dakika ya 114 kwa Bao la
Miaaz Abdelrahim na kupata Bao la usjindi kwenye Dakika ya 118 lililofungwa na
Salah Ibrahim.
Mechi za kusaka Mshindi wa Tatu, kati ya Kili
Stars na Zambia, na Fainali, kati ya Kenya na Sudan, zote zitachezwa Nyayo
Stadium hapo Desemba 12.
VIKOSI:
Kenya:Duncan Ochieng, Allan
Wanga, James Situma, Aboud Omar, Jockins Atudo, Peter Opiyo, Francis Kahata,
Anthony Akumu, Clifton Miheso, David Ochieng Owino, Edwin Lavatsa.
Akibas: Jerim Onyango, Musa Mohammed, Paul Muigai
Kiongera, Ndetto Mulinge, Noah Wafula, David King'atua, David Gateri, Jacob
Keli
Kili Stars: Ivo Phillip Mapunda,
Kelvin Yondani, Edward Erasto Nyoni, Pius Michael Aidan, Frank Raymond Domayo,
Saleh Dilunga, Ally Samata Mbwana, Alfan Mwrisho Ngasa, Thomas Ulimwengu,
Ramadhan A. Kiemba.
Akiba: Bonevetur Munish, Idd Athuman, Mao Himid
Mkami, Athuman Chanongo, Yahaya Singano Shah Raid Mussa, Ismail Adan Gambo,
Maguli Hassan Mrugau
Refa: Thiery Nkurunziza (Burundi)
0 Response to "CHALENJI CUP: FAINALI KENYA v SUDAN! "
Post a Comment