Latest Updates

HAWA NI WASANII TISA AMBAO HAWANA NIDHAMU TANZANIA.


1. T.I.D
Kauli mbaya na dharau ni kawaida kwake maneno kama m.....nge,k......ma na nk yanauhusiano mzuri na mdomo wake.



2. Chidy Benz
Ukisikia kampiga mtu alafu ukashangaa basi utakua mgeni nchini na labda kama hujawai kumsikia msanii huyu.ngumi ndio maisha yake sitoshangaa akiingia kwenye masumbwi mda wowote.alama ya nondo iliyopo upande wa kulia wa kichwa chake ndio ishara tosha ya misukosuko anayokumbana nayo

4. Lord Eyes
Unga unga unga huo ndio wimbo unaomfanya msanii huyu acheze michezo ya wizi kila kukicha ni umaarufu tu unamuokoa watu wanashindwa kumtenda vibaya sababu wanamjua mfano ommy dimpoz aliamua kumpotezea tu kisa anamfahamu.

5. Hemed
Alipokua tusker project fame aliwai kujibizana na jaji ian kiasi cha kutaka kupigana .kifupi ni mtu asiefikiria kabla ya kuzungumza anaweza kukujibu jibu lolote bila kutambua kama yy ni star. Bado hajakua uvumilivu wa kiutu uzima hana mropokaji mzuri sana

6. Dully Skyes
Matusi kwake ni kawaida na dharau kidogo hasa za mdomoni na pia ukiwa unamuhoji kua makini maana anaweza akaongea neno baya redioni bila shaka aliwai kumtongoza dj fetty hewani na kumtukana suddy brown hewani lakini ni muelewa kwani baadae aliomba radhi uswahili na kukosa shule tu vinamsumbua

7. Afande Sele
Kila mtu kagombana na mtu huyu hio ni story ambayo ipo kila kona ya mtaa kuhusu mtu huyu anaongea kwa busara ila akipata mambo yake anaweza kufanya jambo ambalo litakufanya ufikiche macho kuhakikisha kama kafanya yeye au mtu mwingine aliwai kutishia kuua,kuvua nguo jukwaani, na nk

8. Matonya
Huyu yeye ni utapeli tu ndio tatizo lake ukimpa hela ya show kua nae makini sana

9. Mh. Temba
Ukiwa una sikiliza nyimbo ya huyu jamaa usikae na mtu mzima maana utaaibika tu matusi ni moja ya vitu anavyopenda kuvitamka na haonyeshi dalili ya kubadilika kila siku


                                              from D'JARO  

0 Response to "HAWA NI WASANII TISA AMBAO HAWANA NIDHAMU TANZANIA."

Post a Comment