MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini Darasa amefanikiwa kuachia kanda
mseto 'Mixtape' yenye nyimbo 19 aliyoipa jina la 'Dream Big-Chapakazi'
ikiwa inasauti za wasanii mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya akiwemo
Shilole, Ngwear, Mchizi Moxie.
Akielezea dhumuni la kuachia kanda mseto hiyo alidai kuwa ni moja ya
kuupeleka muziki mtaani huku akiwahimiza vijana kuutumia muziki huo kwa
nia ya kujikomboa.
Alidai kuwa kanda hiyo itasambazwa nchi nzima ili ujumbe ufike kwa jamii
nzima hususani vijana ili waweze kuutumia muziki huo kwa lengo la
kujikomboa na kuutendea kazi muziki huo.
Mbali na hilo alidai kuwa bado anaendelea kutoa fulsa kwa vijana katika
kuukuza muziki huo kwa kutoa nafasi kwa baadhi ya vijana ambao wapo
mitaani kwa kushirikiana kufanya nao kazi ambazo zitaingia katika kanda
hiyo.
Alidai kuwa ameamua kuanzisha utaratibu huo wa kuwashirikisha vijana
katika kazi hiyo ili kutoa nafasi kwa vijana hao ambao wanavipaji ila
bado hawajapata fursa ya kukuza vipaji vyao.
0 Response to "DARASA ATOKA NA MIXTAPE VOL 1. "
Post a Comment