MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini Sarah Kaisi 'Shaa' ameweka wazi
kuwa nyimbo yake aliyoitoa hivi karibuni inayojulikana kwa jina la
'Sugua Gaga' imevunja rekodi kwa kuangaliwa na watu zaidi ya elfu 20,000
kwa muda wa siku tatu.
Akizungumza na mwandishi wa habari hili msanii huyo aliweka wazi kuwa
nyimbo hiyo imevunja rekodi ambayo haijawahi kutokea katika kazi zake za
muziki hali ambayo inampa nguvu ya kuona mashabiki wanafwatiria kazi
zake na kuzikubali.
Akielezea sababu ya wimbo huo kuvunja rekodi hiyo Shaa aliweka wazi kuwa
ubunifu wa video hiyo na jisni alivyoimba ndio sababu pekee ilionesha
ubora wa kazi hiyo.
Alisema kuwa ni mmoja kati ya wasanii wanaopokea mabadiliko na kuimba
kutokana na mazingira yoyote anayokutana nayo hali inayompa uzoefu na
kumjenga kwenye kazi yake hiyo ya muziki.
Akielezea wazo la wimbo huo alidai kuwa ni wimbo huo amekuta teyari
umeshatungwa na ilikuwa wazo la Saidi Fella ambapo aliyekusudiwa
kuimba alikuwa ni kijana wa kiume lakini kutokana na uwezo wake aliweza
kuumudu wimbo huo na kuufanya kuwa wake.
"Mimi wimbo nilikuta teyari umeshatungwa kila kitu na alitakiwa kuimba
mwanaume lakini mimi nikapewa ilinichukua siku mbili kuufanyia mazoezi
na kuumudu wimbo huyo" alisema Shaa.
Nyimbo hiyo ya 'Sugua Gaga' imetengenezwa chini ya udhamni wa Mkubwa na Wanawe.
0 Response to " SHAA ATAMBA SUGUA GAGA KUVUNJA REKODI"
Post a Comment